Blogger Tips and TricksLatest Tips And TricksBlogger Tricks
Showing posts with label Jokate. Show all posts
Showing posts with label Jokate. Show all posts

Padri Amtolea Tamko Mrembo Jokate...Ni Kuhusu Kuwakera Waumini Kwa Kupiga Picha za Nusu Utupu

Baadhi ya watu waliodai kuwa wao ni waumini wa Kanisa la Mtakatifu Petro, Oysterbay jijini Dar es Salaam ambako anaabudu Mbongo Fleva na Miss Tanzania No. 2, 2006, Jokate Mwegelo ‘Kidoti’ wamesema nyota huyo hatakiwi kushiriki ibada kwa vile uhusiano wake na Mbongo Fleva, Ali Kiba upo wazi sana, sasa kanisa hilo limetoa tamko, tambaa na Amani.

Akizungumza na gazeti hili juzi kanisani hapo, padri aliyejitambulisha kwa jina moja la Edward ‘Faza Edward’ alisema wao kama kanisa wanamtambua Jokate kama muumini wao wa miaka mingi na kwamba mambo mengine hayawahusu.

“Jokate namtambua kama muumini wetu hapa ana anashiriki vizuri tu. Sisi hatuna tatizo naye. Kwanza sisi  mtu yeyote anaruhusiwa kuja kusali hapa, hata kama ni Mwislam ilimradi tu afuate taratibu zetu.

“Kwa hiyo Jokate tunaye hapa kanisani na anaendelea vizuri tu. Umemuulizia na paroko, yeye muda huu ana wageni,” alisema Faza Edward.


Awali waumini hao walisema kuwa, kitendo cha Jokate kuonekana kwenye vyombo mbalimbali vya habari akiwa na Kiba huku si mwanandoa wake jambo ambalo wao wanaliona si sawasawa kwa vile mrembo huyo hushiriki pia kuimba kwaya ya kanisa hilo.
Mwaka jana, gazeti dada na hili, Ijumaa liliandika habari yenye kichwa kisemacho; Waumini: Jokate anatutia aibu.

Katika habari hiyo, Jokate alidaiwa kuwakera waumini wenzake kufuatia kupiga picha za nusu utupu na kuzisambaza kwenye mitandao ya kijamii huku midume ikijirushia na kujifaidia kwa macho.
Pia, alilalamikiwa kwa tabia yake ya kupanda jukwani kwenye kumbi za muziki na kunengua huku yeye akiwa ni mwanakwaya wa kanisa hiyo.

Akijitetea kuhusu madai ya waumini wenzake katika habari hiyo, Jokate alisema kuwa, kanisa hilo halimzuii kuvaa nguo fupi wala kukata mauno jukwaani kama mwanamuziki kwani kazi ni kazi.
Alisema kanisani anakwenda kama kawaida na kwaya anaimba kama ‘kawa’.
Katika habari hii mpya, Jokaye alipoulizwa alisema: “Mimi sitaki mnifuatilie mambo yangu ya imani, sitaki kabisa, mnanikwaza.”

Waandishi Hamida Hassan na Imelda Mtema.
Global Publishers 3

Mimba ya Jokate Yazua Balaa, Familia Yashtuka

Kwani kimenuka? Siku chache baada ya kubumburuka kwa habari ya kunasa mimba ikimhusisha ‘mtoto mzuri’ Bongo, Jokate Mwegelo ‘Kidoti’ huku mhusika mkuu akitajwa kuwa ni msanii nguli wa Bongo Fleva, Ali Kiba, ishu hiyo imezua balaa kufuatia familia ya mrembo huyo kushtushwa na hali hiyo, Ijumaa Wikienda limenyetishiwa.

TWENDE OYSTERBAY
Mwishoni kwa wiki iliyopita, ‘kijumbe’ wa gazeti hili alitua getini nyumbani kwa akina Jokate, Oysterbay jijini Dar kwa lengo la kutaka kujua nini kinaendelea juu ya binti yao kunasa mimba nje ya ndoa ilihali familia hiyo inasifika kwa misingi bora na maadili ya kidini.

Gazeti hili lilipotia timu nyumbani hapo, lilifanikiwa kuzungumza na mmoja wa wanafamilia hiyo aliyekuwa nje akifanya usafi ambaye bila simile ‘alifunua kinywa’ na kuweka hadharani mambo mazito.

GAZETI LA IJUMAA LAIBUA MAMBO
Kama anayeogopa jambo fulani, memba huyo wa familia ya Jokate alisema kuwa, mrembo huyo alikuwa akifanya siri kubwa juu ya ujauzito wake huo, lakini baada ya gazeti pacha la hili, Ijumaa, kuibua habari hiyo, familia hiyo, hususan mama yake mzazi (jina lipo), alizua utata mkubwa kwa binti huyo na kwamba alishtushwa na hali hiyo na kumlazimu kumkalisha ‘kitako’ Jokate ampe ukweli.

“Jokate alikuwa akifanya siri sana, lakini ninyi mlipoandika habari hiyo, hapakutosha, mama yake alimuitisha kikao na baadhi ya ndugu wengine, lakini Jokate hakutaka kuweka wazi juu ya hali hiyo.

“Ninavyosikia, kuna uwezekano mkubwa wa Jokate kuhama hapa nyumbani akajitegemee ili kuififisha aibu hii kwani familia inadai amewatia aibu kwa kitendo chake cha kubeba mimba nje ya ndoa,” alidai mhusika huyo.

JOKATE ATOWEKA
Mnyetishaji wetu huyo aliendelea kudai kwamba, baada ya kuona anabanwa, alitoweka nyumbani hapo kwa siku mbili kabla ya kurejea na kuondoka kisha kurejea tena.

Kama kawaida ya gazeti hili kujiridhisha kwa kila habari kabla ya kuichapisha na kuwapelekea wasomaji wake, ‘kiranja mkuu’ wa dawati la Ijumaa Wikienda, mashine kubwa kwa habari za ndani za mastaa wa Kibongo, alimtafuta mrembo huyo kupitia simu ya mkononi na alipobaini kuwa mpigaji ni mwandishi wetu alishindwa kusema chochote zaidi ya kuiacha simu hewani na baadaye kuikata.

ATUMIWA SMS
Hata hivyo, ili kujizolea ushahidi madhubuti, mwanahabari wetu alimtumia ujumbe mfupi wa maandishi (sms) na kumsomea madai hayo, lakini hakujibu ujumbe huo licha ya simu ya mwandishi wetu kuonesha kuwa ujumbe ulikuwa umepokelewa (delivered).

KIBA KIMYAA
Pia, kwa upande wa Ali Kiba, simu yake ilionekana kutokuwa hewani muda mwingi, lakini mwandishi wetu alituma ujumbe wa kutaka kusikia chochote kutoka kwake ili akiiwasha simu akutane na ujumbe huo, lakini hadi gazeti hili linaenda kuchapishwa, hakuwa amejibu ujumbe huo achilia mbali kupiga simu hivyo jitihada zinaendelea.

Hata hivyo, mashabiki wa mastaa hao wameendelea kuwapongeza kwa namna ambavyo wamekuwa wakioneshana mahaba na kwamba suala la kupata mtoto ni jambo la heri bila kujali wamefunga ndoa au la.

Chanzo: GPL 3

Nakukutanisha na Video inayoashiria kuwepo mapenzini Jokate na Alikiba.

jojo
Mchana wa jana Aug 14 kwenye kipindi cha XXL kwenye kipengele cha You heard alisikika Alikiba na ilikua ni baada ya kusemekana wazazi wa Jokate hawajawa tayari kumuozesha binti yao Jokate kwa sababu Alikiba muislam wakati Jokate ni mkristu.
jojo2 
Saa chache zilizopita mrembo Jokate amepost picha ikimuonyesha Alikiba akiimba kisha akaipa maneno ‘My Everything‘ picha hiyo imepata comment nyingi na comment nyingi zimwasifia kuwa wanaendana hivyo waweke wazi’
Hii ni video aliyopost Jokate.

3

Crazy Fans of Wema, Kiba and Jokate to vote for Davido

Hivi watanzania mna masaibu gani. Kuna watu wanadai diamond ana dharau, sasa hyo dharau mnaiona mashabiki wa Wema tu. Nimepita pita kitaa kuuliza watu na wanasema hawana tatizo na Diamond.
Ila nimekuja kujua kumbe chanzo cha chuki ni mimba ya zari na kuachana na wema. Washabiki wa wema hawajakubali hali ya wema kutokuwa na raisi wa wasafi, pia Wema nae bado ana kisasi, na ndo mana anaendesha kampeni ya kumpigia kura Davido na sio mtanzania mwenzake Diamond.
Ila tu nisisitize; Jokate, Wema na Mange, nyie na washabiki wenu mpigien Davido wenu, ila msitake kufanya watanzania wengine wamchukie Diamond bila sababu. Sisi watanzania wengine tutampigia kura.
Na naona Vanesa nae ashaanza kuingia team Wema, mana anajipigia promo yeye mwenyewe na kumuacha Diamond, badilika dada.
Vote for Diamond ana Vanesa, MTV Awards.
By Mdau
3

Wema Sepetu na Jokate Mwegelo Waongea Lugha Moja Kusherehekea Ushindi wa Alikiba!

Alikiba na Jokate wanadaiwa kuwa na uhusiano. Wema amekuwa upande wa Kiba tangu kuachana na Diamond na wengi wamekuwa wakikichukulia kama ni kisasi.
Baada ya ushindi huo warembo hao walitumia Instagram kutoa pongezi zao.
“Hongera sana cherie @officialalikiba kwa kujishindia tuzo sita jana usiku kwenye kiba Tanzania music awards (KTMA) sorry Kilimanjaro Tanzania music awards 2015. Teh teh the,” aliandika Jokate.
“Ni kitu cha kumshukuru Mungu ulikaa kimya miaka 3 ila ukarudi na wimbo mmoja ukatuteka tena. Kusema ukweli tukiachilia mbali ushabiki ‘mwana’ ulituliza akili na ukafanya vizuri sana nchini. Mashabiki wanakupenda. Sana. Mpole hivi, mcheshi, mstaarabu. Na unajua mziki. Tunakuombea sasa hii iwe motisha ya wewe kufika mbali zaidi. Ndio kwanza safari imeanza. Uzuri unaomba mungu so najua hata kutupa. Ila kaza mwana we kazaaa!!! We are behind you,” aliongeza.
Naye Wema aliandika: Nilitaka zote saba ila hata 6 pia sio mbaya…. #KingKiba…. Umetisha.”
Jokate pia amepost picha akiwa na Wema na kuandika: It’s a beautiful and powerful thing when strong girls come together. emojiemojiemoji️. With The Sweetheart @wemasepetu
3

Jokate Mwegelo afunguka kwa mara ya kwanza kuhusu uhusiano wake na Alikiba

Kila mtu anaamini kuwa Jokate Mwegelo na Alikiba ni mtu na mpenzi wake japo wao hawajathibitisha hilo rasmi licha ya kupost tu picha zao kwenye Instagram na hivyo kukuza zaidi tetesi hizo.

Lakini hatimaye Jokate amefunguka kwa mara ya kwanza kupitia mahojiano yake na Global TV.


  • “Ni kwasababu Alikiba anapenda sana muziki na anajua muziki na anajua style mbalimbali. Halafu ukitaka kuwa the best you obviously need to be around with the best,” alisema Jokate kujibu swali la uhusiano alionao na King Kiba.



  • “Mimi kwanza ni mchanga, kwahiyo nakaa naye karibu ili niweza kujijenga kimuziki, that is it.”


Sounds kama si jibu tunalohitaji kulisikia! 3

Jokate Mwegelo: Yaani Watu Wangu Mjue Mwanamziki Ali Kiba Ndio Kila Kitu Kwangu...ila....

Mrembo Jokate Katika Pozi
Na Musa Mateja
MREMBO mchakarikaji Bongo,  Jokate Mwegelo ‘Kidoti’, juzikati aliamua kuvunja ukimya na kusema kuwa mwanamuziki Ali Kiba kwa sasa ndiye kila kitu katika mambo yake mengi ya kimaisha.

Akizungumza na Ijumaa Jokate alisema, watu wanaongea sana kuhusiana na ukaribu wao bila kujua kuwa Kiba ni mtu wake kitambo na sasa ndiye kila kitu kwake kwani ana projekti naye kibao ambazo zinakuja na wasioelewa, ipo siku wataelewa.
Mwanamuziki Ali Kiba

Yaani watu wangu wajue Kiba ni kila kitu kwangu ila siyo ishu ya mapenzi, tuna projekti kibao, nawaomba watu wavute subi--ra watajionea kila kinachoendelea kati yetu.Kuanzia sasa Kiba atakuwa akipeperusha ‘brand’ za Kidoti kwa kila atakachofanya ikiwa ni pamoja na mavazi,” alisema Jokate.3

ALI KIBA NA JOKATE Penzi ni Kikohozi Uwezi Kulificha, Wathibitisha Uhusiano wao kwa Picha Hizi

Fresh Jumbe aliwahi kusema penzi ni kikohozi kulificha huwezi.
Na sasa penzi la Jokate Mwegelo na Alikiba limefikia hatua ambayo haliwezi kuwa siri tena. Wawili hao wamekuwa wakidaiwa kuwa wapenzi kwa miezi kadhaa sasa lakini bado binafsi hawajeza kukubali wala kukataa.

Lakini sasa huenda hatua za awali za kuelekea kuuweka hadharani uhusiano huo zimeanza kufanyika. Alianza Jokate aliyepost selfie kwenye Instagram akiwa na msanii huyo aliyejipa jina la King Kiba na kutoandika chochote. Picha hiyo imepata likes 13,215 na comments 824.

Naye Kiba jana alipost selfie nyingi kwenye akaunti yake ya Instagram na kuandika: Pop It In @jokatemwegelo #KingKiba.” Picha hiyo imevutia likes 8108 na comments 680.

Huenda picha hizo zikawa ni tangazo rasmi la uhusiano wao. Kuna tatizo moja lakini – Jokate aliwahi kuwa mpenzi wa Diamond Platnumz!

JE JOKATE NAFANYA HIVYO KUMUUMIZA DIAMOND? 3
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Hapa Chini

 
Support : Gallos official blog | Gallos official blog | Gallos official blog
Copyright © 2011. Gallos official blog - All Rights Reserved
Modified by Yuvinusm
Powered by Blogger
Tricks and Tips