Blogger Tips and TricksLatest Tips And TricksBlogger Tricks
Home » » Sakata la Gwajima: Serikali Inapoamua Kukumaliza Baada ya Kuchanganya Dini na Siasa

Sakata la Gwajima: Serikali Inapoamua Kukumaliza Baada ya Kuchanganya Dini na Siasa

Ishu ya Gwajima ni kama ndio imeanza upya baada ya kutakiwa kuleta nyaraka kumi muhimu, zikiwemo returns za hesabu zake za kanisa, bodi ya wadhamini, hati ya usajili wa kanisa, namba ya utambulisho, jumla ya makanisa yake, mali anazimiliki nk 
Kwa juu juu ni rahisi kuona hili ni jambo jepesi lakini kiuhalisia huu unaweza kuwa mwanzo wa mwisho wa enzi za gwajima. Kila nyaraka atakayoleta itachambuliwa kwa vigezo vyote na kwakweli nyingi ya nyaraka hizo (kama zitakuwepo) zitakuwa na mushkeli
Na mushkeli utakaotokea kwenye kila nyaraka utaangaliwa kwa jicho la kisheria na adhabu zake, hii ni msiba kwa yoyote yule ambaye anafanyiwa ukaguzi na serikali, yataibuka mengi mengi ambayo hayajulikani, kuanzia mamlaka ya mapato, vyeti na usajili, uhamiaji, taratibu za kuendesha kanisa nk nk
Pamoja na kashfa zake nyingi lakini hii ishu ni ya kisiasa zaidi, na hii inatokana kuweka wazi msimamo wake bila woga wa kuwaunga mkono watu wawili muhimu kwenye uchaguzi mkuu ujao Lowassa na Dr Slaa, hawa wawili hawa ni homa mbaya kwa ccm kwasasa, yeyote atakayefanikiwa kuchukua madaraka ni kiama kwa ccm, japo El yupo ccm
Gwajima anaponzwa na kujiamini kulikopitiliza na kuchanganya na siasa za makundi, hawatamuacha hadi wahakikishe wamemmaliza kabisa
WEKA MAONI YAKO HAPA CHINI
Weka e-mail yako hapa kupata habari moja kwa moja Karibu sana Usikose kupata habari kwa kutembelea blog yetu Gallos official blog

0 comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Hapa Chini

 
Support : Gallos official blog | Gallos official blog | Gallos official blog
Copyright © 2011. Gallos official blog - All Rights Reserved
Modified by Yuvinusm
Powered by Blogger
Tricks and Tips