Baada ya Zitto kutoa kauli kwa vyombo vya habari kuwa, kuna zaidi ya
wabunge 50 kutoka vyama vya CCM na CHADEMA watakao hamia ACT, CHADEMA
kupitia kitengo chake cha intelijensia kimetangaza upelelezi rasmi ili
kuweza kuwavumbua wabunge hao wasaliti wa chama na mamluki wengine!
Aidha, maofisa hao katika kitengo hicho cha intelijensia cha CHADEMA
wameeleza wazi kuwa wanaifanya kazi hiyo kwa usahihi na umakini mkubwa
ili kuhakikisha taarifa watakazokusanya ni za kweli huku wakielezea
mkakati wao wa kupenyeza watu wao ndani ya ACT kwa ajili ya taarifa
zaidi!
My take,
Kwa hali hii, nadhani CHADEMA imeanza kusahau jukumu lake la msingi la
kufanya siasa na kujenga chama, badala yake nguvu nyingi zaidi
imeelekezwa kwenye kusaka hao wanaoitwa 'wasaliti'!
Mbona CCM ina watu wanatofautiana kimtazamo lakini maisha ya siasa
yanaenda kama kawaida na hatusikii majina majina kama wasaliti?
WEKA MAONI YAKO HAPA CHINI
.jpg)
0 comments:
Post a Comment