Blogger Tips and TricksLatest Tips And TricksBlogger Tricks
Home » » Mahakama ya Misri imeamua adhabu hii kwa Rais wao wa zamani!!

Mahakama ya Misri imeamua adhabu hii kwa Rais wao wa zamani!!

mosi
Makahama ya Misri imetoa hukumu kwa aliyekuwa Rais wa nchi hiyo Mohammed Morsi  kutokana na kuuawa kwa waandamanaji wengi wakati akiwa madarakani.
Hukumu hiyo iliolewa leo kwa Rais huyo tangu aondoke madarakani mwaka 2013 kufuatia maandamano makubwa mitaani ya kupinga uongozi wake sasa amehukumiwa jela miaka 20.
Yeye pamoja na viongozi wengine wa Muslim Brotherhood walilaumiwa kwa kuwachochea wafuasi wao kumuua mwandishi wa habari na waandamanaji wa upinzani wakati wa vurugu nje ya ikulu ya nchi hiyo mwishoni mwa mwaka 2012.
Wakati umati ulipokusanyika nje ya ikulu bwana Morsi aliwaamrisha polisi kuwatawanya lakini wakakataa kufanya hivyo.
mahakamanBaadaye Muslim Brotherhood waliwaleta wafuasi wao ambapo watu 11 waliuawa kwenye vurugu hizo, wengi kutoka kundi la Muslim Brotherhood.
Kabla ya kutolewa hukumu  leo, Muslim Brotherhood walimlaumu rais wa sasa Abdul Fatta al-Sisi kwa kutumia mahakama kama silaha.
WEKA MAONI YAKO HAPA CHINI
Weka e-mail yako hapa kupata habari moja kwa moja Karibu sana Usikose kupata habari kwa kutembelea blog yetu Gallos official blog

0 comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Hapa Chini

 
Support : Gallos official blog | Gallos official blog | Gallos official blog
Copyright © 2011. Gallos official blog - All Rights Reserved
Modified by Yuvinusm
Powered by Blogger
Tricks and Tips