Blogger Tips and TricksLatest Tips And TricksBlogger Tricks
Home » » ROSE MHANDO Amkimbia Meneja Wake

ROSE MHANDO Amkimbia Meneja Wake

NYOTA wa nyimbo za Injili Bongo, Rose Muhando anadaiwa kumkimbia meneja wake, Alex Msama licha ya kuwepo kwa makubaliano kati yao yaliyohusu kulipiwa deni la kiasi cha shilingi milioni sita alizokuwa akidaiwa msanii huyo mwenye jina kubwa.

Alex Msama ambaye ni meneja wa Rose muhando.

“Meneja wake alikubali kumlipia pesa zote (6,500,000) ambazo Rose alikuwa anadaiwa baada ya kushindwa kuhudhuria tamasha moja huko mikoani, alitakiwa baada ya siku chache aingie studio kufanya kazi, lakini ametoweka na haifahamiki yupo wapi,” kilisema chanzo chetu.

Msama alipotafutwa alikiri kutokea kwa tukio hilo, akisema haeleweki Rose ana matatizo gani kwani walikubaliana baada ya siku chache aingie studio na kurekodi, lakini mpaka hivi sasa haijulikani alipo na hata simu yake ya mkononi haipatikani.
GPL

Gazeti hili lilimtafuta Rose bila mafanikio kwani simu yake haikuwa hewani. WEKA MAONI YAKO HAPA CHINI
Weka e-mail yako hapa kupata habari moja kwa moja Karibu sana Usikose kupata habari kwa kutembelea blog yetu Gallos official blog

0 comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Hapa Chini

 
Support : Gallos official blog | Gallos official blog | Gallos official blog
Copyright © 2011. Gallos official blog - All Rights Reserved
Modified by Yuvinusm
Powered by Blogger
Tricks and Tips