Wakati Dar es salaam Tanzania bado inasubiri kuanza kufanya kazi kwa mabasi yaendayo haraka, sasa hivi nakupeleka moja kwa moja kwenye jiji la Barcelona Spain, jiji ambalo mpaka mwaka 2011 lilikua na watu zaidi ya milioni moja na laki sita ndani yake na sasa wanasema kuna zaidi ya watu milioni 5 ambapo ni jiji la pili kwa ukubwa kwenye nchi ya Hispania.
Hizi zilitumika Hispania kwenye miaka ya 1960 baada ya kuchukuliwa baada ya kutumika Washington Marekani
Kwenye hii picha ya juu na ya chini ni
muonekano wa Tram za mwanzoni kabisa wakati Barcelona imeanza kutumia
aina hii ya usafiri.
Baada ya mapito yote hayo sasa hivi mji wa
Barcelona unatumia Tram za kisasa zinazopita kwenye njia yake ya reli
kama kawaida na wamezitengenezea sehemu yake iliyo na mvuto zaidi kama
unavyoona kwenye picha hapa chini na barabara hiyo usafiri mwingine
wowote hauruhusiwi kupita.
zinapita chini ya ardhi na kusafirisha watu kwenda sehemu mbalimbali ndani ya mji, ni usafiri maarufu kwa jina la Metro.
Mfumo wa nauli kwenye Treni hizi za chini
maarufu kama Metro unatumia kadi kama za ATM ambazo unaweza kulipia
safari nyingi na ukifika kwenye mlango wa kuingilia kama huu hapa chini
unaipitisha ile kazi kisha mlango unakuruhusu kupita kuingia kwenye
kituo na kupanda Treni ya safari yako.
Hii
ni sehemu ya kutazama vituo na maelekezo ya unakokwenda, mchoro huu upo
kwenye vituo vya Treni hizi pamoja na ndani ya Treni zenyewe, ukitaka
kujua unaposhukia kuna taa huwa inawaka kwenye viduara vyenye majina ya
vituo so inakujulisha tuko kituo gani kwa sasa na kituo kinachofata
Hapa chini nimekuwekea video inayoonyesha jinsi ya kununua Ticket, na usafiri wenyewe ulivyo.
Kumbuka hii ni chini ya ardhi, Metro huwa zinatumiwa na watu wengi sababu hakuna foleni na sasa usalama upo japo kuna wale Wanawake wa Romania wanaotajwa sana kuibia watu mifukoni ndani ya hizi Treni, ukiachia hiyo huu ni usafiri salama wa kuutumia na hamna wezi wa kukaba hata iwe usiku wa saa ngapi.
WEKA MAONI YAKO HAPA CHINI
0 comments:
Post a Comment