

Tumepokea kwa udhuni na majonzi makubwa taarifa ya kifo cha mkongwe wa muziki wa dansi nchini Tanzania na
Africa ya mashariki marehemu mzee Muhidin Maalimu Gurumo Kilichotokea leo 13.04.2014 huko nyumbani Tanzania.Pamoja na kuwa mbali na nyumbani bendi ya muziki wa dansi Ngoma Africa Band yenye makao yake nchini Ujerumani inaungana na watanzania wote popote pale katika kuomboleza msiba huu.Tunatoa pole zetu kwa bendi ya Msondo Ngoma pamoja na familia ya marehemu,mwenyezi munguamlaze mahala pema peponi marehemu Mzee Muhidin Maalim
Gurumo (RIP)Amina
0 comments:
Post a Comment