Blogger Tips and TricksLatest Tips And TricksBlogger Tricks
Home » » Houthi washambulia Saudi Arabia

Houthi washambulia Saudi Arabia

Mpiganaji wa Houthi
Saudi Arabia inasema kuwa imezuia makombora yaliyofyatuliwa kutoka nchini Yemen kwenda ardhi yake na waasi wa Houthi.
Utawala unasema kuwa makombora hayo yalikuwa yamelenga mji wa Khamees Mushait mapema leo lakini yakadunguliwa .
Waasi wa Houthi
Mashambulizi hayo yalifanyika baada ya Saudi Arabia kuripoti mapigano yaliyodumu saa kadha siku ya Ijumaa maeneo ya mpaka ya Jizan na Najran.
Shirika moja la habari lilisema kuwa raia wanne wa Saudi Arabia waliuawa na watu wengine kadha nchini Yemen wakati jeshi lilipopambana na waasi wa Houthi watiifu kwa rais wa zamani ya Yemen Ali Abdullah Saleh.
Wakazi wa mji mkuu Sanaa wanasema kuwa mji huo baadaye ulishambuliwa vikali na muungano unaoongozwa na Saudi Arabia.

    Gallos Official Blog

Chanzo BBC
WEKA MAONI YAKO HAPA CHINI
Weka e-mail yako hapa kupata habari moja kwa moja Karibu sana Usikose kupata habari kwa kutembelea blog yetu Gallos official blog

0 comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Hapa Chini

 
Support : Gallos official blog | Gallos official blog | Gallos official blog
Copyright © 2011. Gallos official blog - All Rights Reserved
Modified by Yuvinusm
Powered by Blogger
Tricks and Tips