Blogger Tips and TricksLatest Tips And TricksBlogger Tricks
Home » , » Kingine kilichosikika kutoka Kenya kuhusu shambulio la Chuo Kikuu, kiongozi wa Serikali kahusishwa na uzembe..

Kingine kilichosikika kutoka Kenya kuhusu shambulio la Chuo Kikuu, kiongozi wa Serikali kahusishwa na uzembe..

img_9541 
Siku chache zimepita toka lilipotokea tukio la kigaidi katika Chuo cha Garissa Kenya, kwenye tukio hilo wanafunzi 148 walifariki.. kingine kilichonifikia leo April 10 toka Kenya kinahusu uchunguzi uliofanyika kuonesha kwamba kuna dalili za uzembe ama matumizi mabaya ya madaraka wakati wa mikakati ya kupambana na wavamizi hao.
Taarifa za kwenye vyombo vya habari Kenya zinasema ndege ambayo ilitakiwa isafirishe maafisa wa Polisi kwenda kwenye Chuo hicho kwa ajili ya kupambana na wavamizi hao ilitumiwa kwa ajili ya safari binafsi ya familia moja ambapo kuna kiongozi mmoja anahusishwa kuruhusu ndege hiyo kufanya safari hiyo wakati ambao ilitakiwa kuwapeleka maafisa hao Garissa.
Rubani amesema ndege hiyo iliondoka katika uwanja wa ndege na kuwaacha makomandoo wa RECCE wakisubiri irudi kuwachukua na kuwapeleka Garissa kuwaokoa wanafunzi.
 Nimekuwekea taarifa hiyo hapa iliyoripotiwa na kituo cha  K24 bonyeza play kuisikiliza… WEKA MAONI YAKO HAPA CHINI
Weka e-mail yako hapa kupata habari moja kwa moja Karibu sana Usikose kupata habari kwa kutembelea blog yetu Gallos official blog

0 comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Hapa Chini

 
Support : Gallos official blog | Gallos official blog | Gallos official blog
Copyright © 2011. Gallos official blog - All Rights Reserved
Modified by Yuvinusm
Powered by Blogger
Tricks and Tips