Blogger Tips and TricksLatest Tips And TricksBlogger Tricks
Home » » Mwana wa Mugabe apatikana na hatia

Mwana wa Mugabe apatikana na hatia

Grace Mugabe


Mwana mkubwa wa kiume wa mke wa rais wa Zimbabwe Grace Mugabe amepatikana na hatia ya kuua bila kukusudia na kupigwa faini ya dola 800.
Russell Goreraza alimgonga na kumuua mwanamume mmoja ambaye hakutambuliwa katika gari lake katika mji mkuu wa Harare manmo mwezi Februari.
''Ninajuta na ningependa kuomba msamaha kwa kitendo hicho'', Kijana huyo wa miaka 31 aliimbia mahakama.
Hakimu huyo alisema kuwa aliamua kuifutilia mbali leseni ya kijana huyo na kumpatia hukumu ya kifungo cha jela lakini akabadilisha nia yake kutokana na majuto yake.
Douglas Chikwekwe amesema kuwa hatua kwamba Goreraza alitekeleza kitendo hicho kwa mara ya kwanza pia kuliathiri uamuzi wake.
 
Gallos Official Blog

Chanzo BBC
WEKA MAONI YAKO HAPA CHINI
Weka e-mail yako hapa kupata habari moja kwa moja Karibu sana Usikose kupata habari kwa kutembelea blog yetu Gallos official blog

0 comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Hapa Chini

 
Support : Gallos official blog | Gallos official blog | Gallos official blog
Copyright © 2011. Gallos official blog - All Rights Reserved
Modified by Yuvinusm
Powered by Blogger
Tricks and Tips