Mchezaji
wa raga wa ligi kuu nchini Australia, ambaye alipata majeraha mabaya
katika mchuano wa kuwania kombe la Queensland nchini humo, amefariki
hospitalini.
James Ackerman, mwenye umri wa miakia 25, alikuwa
akiichezea timu ya Sunshine Coast Falcons, alipopata majeraha mabaya ya
kichwa dakika tano tu baada ya kuanza kwa mechi dhidi ya timu ya Norths
Devils.Mchezaji huyo aliye na watoto wawili, alitibiwa katika uwanja wa Bishop Park, kabla ya kukimbizwa Hospitalini mjini Brisbane.
Mechi hiyo iliofanyika siku ya Jumamosi ilisitishwa.
Wakuu wa Queensland Rugby League (QRL) wametangaza rasmi leo Jumatatu kwamba, Ackerman ameaga dunia.
Kwa mjibu wa gazeti la Courier-Mail linalochapishwa mjini Australia , Francis Molo, mwenye umri wa miaka 20, na ambaye alikabiliana na Ackerman na kusababisha majeraha hayo, ameingiwa na wasiwasi mkubwa.
Mkurugenzi mkuu wa Sunshine Coast Falcons, Chris Flannery, amemuelezea Ackerman kama "bingwa" na "mmojawepo wa viongozi wetu".
Chanzo BBC
Gallos Official Blog
0 comments:
Post a Comment