Blogger Tips and TricksLatest Tips And TricksBlogger Tricks
Home » , » Jack Warner aapa kufichua ufisadi FIFA

Jack Warner aapa kufichua ufisadi FIFA

 
Jack Warner amesema atafichua kila anachojua katika FIFA
Aliyekuwa makamu wa rais wa shirikisho la soka duniani FIFA Jack Warner amesema katika hotuba ya kushangaza aliyotoa katika runinga kwamba atafichua kila anachojua kuhusu ufisadi katika shirikisho hilo.
Bwana Warner ambaye alisema kuwa anahofia maisha yake pia amesema kuwa anaweza kuwahusisha maafisa wa FIFA na uchaguzi mkuu katika taifa la Trinidad and Tobbago mwaka 2010.
Maafisa wa FIFA wanaotuhumiwa na ufisadi
Ni mmoja wa watu 14 walioshtakiwa na Marekani kuhusiana na ufisadi katika FIFA.
Mmoja wa maafisa wakuu wa FIFA na shahidi muhimu Chuck Blazer alikubali kuchukua hongo.
Chuck Balzer akiwa na Sepp Blatter
Afisa huyo alikiri kufanya hivyo mnamo mwaka 2013,ikiwa ni miongoni mwa mashtaka yaliofunguliwa ambayo yameikabili FIFA na kumlazimu rais wake Sepp Blatter Kujiuzulu.
Idara ya mahakama ya Marekani inadai kuwa watu 14 walioshtakiwa walikubali hongo ya zaidi ya dola milioni 150 katika kipindi cha miaka 24.
Chuck Blazer amekiri kupokea hongo
Watu wengine wanne walikuwa tayari wameshtakiwa akiwemo Blazer.
                    Gallos Official Blog
Chanzo BBC

WEKA MAONI YAKO HAPA CHINI
Weka e-mail yako hapa kupata habari moja kwa moja Karibu sana Usikose kupata habari kwa kutembelea blog yetu Gallos official blog

0 comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Hapa Chini

 
Support : Gallos official blog | Gallos official blog | Gallos official blog
Copyright © 2011. Gallos official blog - All Rights Reserved
Modified by Yuvinusm
Powered by Blogger
Tricks and Tips