Blogger Tips and TricksLatest Tips And TricksBlogger Tricks
Home » » Donaldo Ngoma kutua Yanga

Donaldo Ngoma kutua Yanga

Donaldo Dondo
Mshambuliaji wa Platinum FC ya Zimbabwe, Donaldo Ngoma anatarajiwa kuwasili Tanzania kwa ajili ya kukamilisha mazungumzo ya kujiunga na mabingwa wa Tanzania Bara, Yanga.
Mchezaji huyo anatarajiwa kuwasili Dar es Salaam muda wowote kuanzia sasa, kwa mujibu wa uongozi wa Yanga.
Yanga, wakiwa na kibarua cha kuiwakilisha Tanzania katika michuano ya ligi ya Mabingwa Afrika mwakani, ipo katika nchakato wa kusajili wachezaji mahiri kwa ajili ya msimu ujao wa 2015/16 wa ligi kuu Tanzania Bara na michuano ya kimataifa. Hatua ya kujiimarisha inakuwa baada ya Yanga kutolewa katika ligi ya Kombe la Shirikisho mwaka huu na timu ya Etoile du Sahel ya Tunisia.
Yanga ilivutiwa na Ngoma wakati ilipocheza na Platimun FC katika mechi za awali za Kombe la Shirikisho mwaka huu na kuitoa timu hiyo kutoka kusini mwa Afrika.

               Gallos Official Blog
Chanzo BBC


WEKA MAONI YAKO HAPA CHINI
Weka e-mail yako hapa kupata habari moja kwa moja Karibu sana Usikose kupata habari kwa kutembelea blog yetu Gallos official blog

0 comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Hapa Chini

 
Support : Gallos official blog | Gallos official blog | Gallos official blog
Copyright © 2011. Gallos official blog - All Rights Reserved
Modified by Yuvinusm
Powered by Blogger
Tricks and Tips